Pages

Subscribe:

Ads 468x60px

Tuesday, March 25, 2014

MAJINA YA WASANII WANAOWANIA "NOMINEES" TUNZO ZA KILIMANJARO TANZANIA MUSIC 2014


Baraza la sanaa Tanzania (BASATA) limetangaza rasmi matokeo ya mchakato wa kuwapata wateule rasmi yaani ‘nominees’ wa vipengele 34 vya tuzo za muziki Tanzania.HAWA HAPA..

Wimbo Bora wa mwaka
Number One – Diamond
Joto Hasira – Jaydee
I love u – Cassim
Yahaya – Lady Jaydee
Kidela – Abdul Kiba
Muziki Gani – Nay wa Mitego

Wimbo bora wa Kiswahili – Band
Ushamba Mzigo – Mashujaa
Shamba la Bibi – Victoria sound
Chuki nini – FM Academia
Yarabi nafsi – Mapacha 3
Kiapo – Talent Band

Wimbo Afro Pop
Number One – Diamond
Joto Hasira – Lady Jaydee
Kidela – Abdul Kiba
I love u – Cassim
Tupogo – Ommy Dimpoz
Roho Yangu – Mavoko

Wimbo bora wa Hip Hop
Bei ya Mkaa – Weusi
Nje ya Box – Nick wa Pili & Joh Makini
Siri ya Mchezo – Fid Q
2030 – ROMA
Pesa – Mr Blue

Wimbo bora wa R&B
Listen – Belle 9
Closer – Vanessa Mdee
So Crazy – Maua Samma
Kama Huwezi – Rama Dee
Wa Ubani – Ben Pol

Wimbo bora wa kushirikisha/kushirikiana
Muziki Gani – Nay wa Mitego f/ Diamond
Joto Hasira – Lady Jaydee f/ Profesa Jay
Kidela – Abdul Kiba f/ Ali Kiba
Bila Kukunja Goti – Mwana FA & AY f/ J-Martins
Tupogo – Ommy Dimpoz f/ J-Martins

Wimbo bora wa Zouk Rhumba
Yahaya – Lady Jaydee
Yamoto – Mkubwa na Wanawe
Msaliti – Christian Bella
Nakuhitaji – Malaika Band
Narudi Kazini – Beka

Mwimbaji Bora wa Kike – Kizazi Kipya
Vanessa Mdee
Lady Jaydee
Linah
Maua Sama

Mwimbaji Bora wa Kiume Kizazi Kipya
Ben Pol
Rich Mavoko
Diamond Platnumz
Ommy Dimpoz
Cassim Mganga

Msanii Bora Hip Hop
Fid Q
Stamina
Young Killer
Nick wa Pili
G-Nako

Msanii Bora Chipukizi
Young Killer
Walter Chilambo
Y Tony
Snura
Meninah

Mtayarishaji Bora – Kizazi Kipya
Marco Chali
Man Water
Mazoo
Sheddy Clever
Nahreel

Mtunzi Bora wa Mwaka – Kizazi Kipya
Belle 9
Ben Pol
Diamond
Rama Dee
Rich Mavoko

Mtunzi Bora Hip Hop
Nikki wa Pili
Young Killer
ROMA
Fid Q
G-Nako

Mtumbuizaji Bora wa Kiume Kizazi Kipya
Diamond
Christian Bella
Rich Mavoko
Ommy Dimpoz
Abdul Kiba

Video Bora ya Mwaka
Number One – Diamond
Yahaya – Lady Jaydee
Joto Hasira – Lady Jaydee
Uswazi Takeaway – Chege
Mama yeyo – GNako

Mtunzi Bora wa Mwaka Band
Christian Bella
Jose Mara
Chaz Baba
Nyosh El Saadat
Kalala Junior

Bendi ya Mwaka
FM Academia
Mapacha Watatu
Twanga Pepeta
Akudo Impact
Malaika Band
Mashujaa Band

Kikundi Cha Mwaka – Kizazi Kipya
Makomandoo
Navy Kenzo
Weusi
Mkubwa na Wanawe
Kikundi cha Mwaka – Taarab
Jahazi Modern Taarab
Mashauzi Classic
Five Stars

Mwimbaji Bora wa Kike – Taaarab
Khadija Kopa
Isha Ramadhani
Khadija Yusuph
Mwanahawa Ali
Leyla Rashid

Mwimbaji Bora Kiume – Taarab
Mzee Yusuf
Hashimu Saidi
Mohamed Ali aka Mtoto Pori

Mwimbaji Bora Kiume – Bendi
Jose Mara
Kalala Junior
Charz Baba
Khalid Chokoraa
Christian Bella

Mtunzi Bora Taarab
Mzee Yusuf
El-Ahad Omary
El-Khatib Rajab
Kapten Temba
Sadiki Abdul
Nassoro Seif

Rapper bora wa mwaka – Bendi
Kitokololo
Chokoraa
Ferguson
Canal Top
Totoo Ze Bingwa

Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka – Taarab
Enrico
Abuu Mwana ZNZ
Bakunde

Mwimbaji Bora wa Kike – Bendi
Luiza Mbutu
Catherine Cindy
Ciana

Wimbo bora wa reggae
Niwe Nawe – Dabo
Hakuna Matata – Lonka
Tell Me – DJ Aron f/ Fidempha
Bado Nahitaji – Chikaka f/ Bless P & Lazzy
Bongo Reggae -Warriors from the East

Wimbo bora wa Ragga/Dancehall
Nishai – Chibwa f/ Nuru
Sexy Girl – Dr Jahson
My Sweet – Jetman
Feel Alright – Lucky Stone
Wine – Princess Delyla

Wimbo bora wa Afrika Mashariki
Tubonge – Jose Chameleone
Nakupenda Pia – Wyre f/ Alaine
Badilisha – Jose Chameleone
Kipepeo – Jaguar
Kiboko Changu f/ Radio and Weasel

VIDEO MPYA YA SHILOLE "CHUNA BUZI"

Video iliyoleta gumzo sana mtandaoni kutokana na matukio yaliyomo kwenye video hii...
   Shilole "Chuna buzi" video

Sunday, March 23, 2014

VIDEO MPYA LADY GAGA "G.U.Y" KUTOLEWA SASA

           Mwanamuziki mwenye vituko sana katika video zake Lady Gaga ameachia  video ya wimbo wake "G.U.Y ( Girl Under You )"video imeongazwa na yeye mwenyewe na ilifanyika kwa siku 6 huko California kwenye hekalu la Hearst Castle.
                                                              

SHAKIRA NDIYE MWANAMUZIKI MWENYE LIKES NYINGI ZAIDI KWENYE FACEBOOK,ZAIDI YA LIKES MILIONI 86

            Mwimbaji mrembo Shakira wa Colombia ndiye mwanamuziki mwenye ukurasa wenye likes au wafuasiwengi zaidi duniani kwa sasa katika mtandao wa kijamii wa Facebook baada ya kufikisha likes 86,549,479. Na kufuatiwa kwa karibu na mwanadada Rihanna aliyeshirikiana naye katika nyimbo iliyofanya vizuri sana "I can't remember to forget you" ambaye ameshika nafasi ya pili kwa kuwa na likes 86,200,046  hukuwa tatu ni mwanamuziki wa mziki wa HIP HOP Eminem mwenye likes 83,904,675 kwa mujibu wa metro.co.uk

Shakira
 Mwanadada Shakira mwenye hit song "Hips don't lie" pia alishare habari hiyo na mashabiki wake wa mtandao huo wa kijamii Facebook kwa kuandika;
"Wow.... i was just told i now have the most followed page on facebook in the world! i still cannot belive it!
i always wanted to have a lot of friends but never imagined it would be so many...86m!
so humbled,can't thanks you guys enough for your support,i feel so fortunate to have you.
Giant kiss! Forever thankful,
Shak
"

Shakira anatarajia kuachia album yake mpya na ya kumi iitwayo 'shakira' jumanne ya wiki hii inayoanza March 35.

Hii ni top ten ya watu maarufu wenye likes nyingi Facebook;
1.Shakira - 86,429,950 likes
2.Rihanna - 86,271,149 likes
3.Eminem - 83,935,160 likes
4.Cristiano Ronaldo - 76,148,074 likes
5.Michael Jackson - 71,605,480 likes
6.Vin Diesel - 70,124,905 likes
7.Katy perry - 65,694,061 likes
8.Will Smith - 64,732,390 likes
9.Justin Bieber - 64,167,390 likes
10.Lady Gaga - 63,776,645 likes

MBEYA FREE MUSIC CONCERT YA ZANTEL WAKISHILIKIANA NA SWEETY FM.

    Onesho lililofanyika mjini Mbeya katika viwanja vya "Mbeya city pub" na kupambwa na MCs kutoka sweety fm kwa ajili ya kukuza vipaji vya wasanii wanaochipukia mjini Mbeya .Msanii mkubwa wa mziki wa HIP HOP kutoka salasala Godzilla a.k.a King zilla ku-perform ndani ya jukwa hilo la Mbeya free music concert lililopambwa na vituko vingi kutoka kwa watoto wa Mbeya city....

Watangazaji wa Sweety fm Langa na Ashrey wakifungua show
 Show ilianzishwa na ma-underground, ma-dancers na wanamuziki kutoka Mbeya city waliovamia jukwaa kwa nguvu zote na kuacha mashabiki kupiga shangwe "non-stop" bila kuchokwa noa, kati ya wanaburudani walio pagawisha mashabiki ni Kareem,Z-kali,ukwu dancer na pia Modolist aliye pagawisha mashabikki zaidi  kwa wimbo wake wa "Usiniache" akifuatiwa na wanadada wa inye ndembendembe kupagawisha, pia burudani kutoka kwa watangazaji wa sweety fm kuwabamba zaidi mashabiki...

Watangazaji wa vipindi vya Sweety fm mbeya wakila bonge la sebene

Ukwu dancers nao hawakuwa nyuma katika kuwaburudisha mashabiki

Wadau wa burudani wakiwa wamefurahia show noma sana
Jukwaa lilipamba moto zaidi pale walipopanda wanamuziki kutoka Mbeya city wakifuatiwa na King zilla kutoka salasala Dar es salaam...wasanii waliokuwepo kutoka Mbeya city ni Kesse boy,Zax B,Jozy  mapenzi,PC the master,MC murder,Must,BZQ na pia mwanadada Lil stiga kwa pamoja ndani ya jukwaa moja na kuwapagawisha mashabiki sana.  

Friday, March 21, 2014

WIMBO MPYA WA LADY JAYDEE KUJA HIVI KARIBUNI

 Mwanamuziki Judith Wambura a.k.a Lady jaydee ameanza kuutangaza wimbo wake mpya unaoitwa  "nasimama" na kusema sio muda mrefu anaachia nyimbo hiyo baada ya "historia". Mwanadada huyo ambaye kabla ametesa sana na wimbo wa "yahaya" ameendelea kuwakimbiza wanamuziki wenzake kwa nyimbo "kistoria" na sasa "nasimama"

Lady Jaydee
Mwanadada huyo aanzakuitangaza wimbo huo kwa ku-post kwenye mitandao ya kijamii
"Chorus ya wimbo wangu mpya ambao haujatoka unaitwa NASIMAMA... maneno haya hapaa"

CHORUS;aliyepanga ni maanani,shida na riziki zangu
aliyezitupa gizani,shida na tabu zangu oooh *2

NYIMBO MPYA DIAMOND PLATNUMZ "KIFO CHANGU"

Mwanamziki namba 1 kwa kupiga show hapa Tanzania Diamond Platnumz hivi karibuni alitoa maneno akizungumza siku akifa itakuwawaje kitu ambacho kilizua maswali mengi sana kwa mashabiki wake ambao hawakutegemea hata siku moja kama atakuja kusema maneno kama hayo kwa mashabiki wake kwani yalizua mining'ono mingi sana. Katika kusema hayo maneno Diamond alisema ni moja kati ya nyimbo ambayo ameiandika na inamtoa machozi kia aisikapo.
Baadhi ya mashairi katika nyimbo hiyo alisema:

                                                 Vipi Maneke atanililia...??
                                                 Je wasanii wenzangu wataniimbia..??
                                                Ama litafutika jina langu...??
                                                Na nyimbo zangu hawatasikia..??
                                                Vipi wasafi watanililia....??
                                                Je ndugu rafiki watahudhuria..?? 
                                                Ama nitakapokufa Sina changu..??
                                               Hata mama yangu watamkimbia...??

Kwa mara ya kwanza pata kuisikiliza na kudownload nyimbo hiyo hapa Diamond-kifo-new song

Wednesday, March 19, 2014

YARIPOTIWA KUWA NCHINI MAREKANI VIJANA WENYE ASILI YA AFRIKA HUCHUKULIWA WANAHATIA.

   Makala iliyo sambazwa na "journal of personality and social psychology" imegundulika kuwa vijana wenye asili ya Africa nchini Marekani huchukuliwa kuwa ndio wenye vurugu na usumbufu katika sheria na kuwafanya kuwa wahanga wa matukio mbalimbali na bila kupewa nafasi ya kujitetea mbele ya polisi kwasababu ya zana hiyo....



Polisi wa nchini Marekani wakimkamata kijana mwenye asili ya Afrika
        "Vijana katika jamii nyingi zinawachukulia vijana kama kundi la watu wasio na hatia na wanaitaji ulinzi kutoka kwa wazazi na jamii kwa ujumla..." asema Phillip Goff ambaye ni mwandishi wa makala hiyo... Profesa huyo akaongezea kwa kusema "utafiti wetu umegundua kuwa vijana wenye asili ya Afrika hawachukuliwi kama wanavyo chukuliwa vijana wazungu" na kufanya polisi kutumia nguvu na pia mbwa wanapoenda kuwakamata vijana kwani ni wenye vurugu kuliko....


Utafiti huo umewapitia kuwahoji polisi zaid ya 176 wengi woa wakiwa ni weupe "wazungu" na hilo ni usibitisho kuwa watu wenye asili ya Afrika kutoaminiwa na sheria au serikari pia na kuchunguzwa kwa karibu zaidi wanapo taka kujiunga na jeshi la polisi... utafiti huo umegundua pia 88% za vijana walio kamatwa na polisi ni wale wenye asili ya Afrika na walatino katika kipindi kifupi tu.

Saturday, March 15, 2014

LIL WAYNE ACHUKIZWA NA KANYE KWA SABABU YA ALBAM YA TYGA.


      LIL WAYNE ACHUKIZWA NA KANYE KWA SABABU YA ALBAM YA TYGA.
 Nyota wa muziki wa HIP HOP nchini Marekani Lil Wayne na pia
muanzilishi na mmiliki wa kundi la "young money" amechukizwa na kitendo cha
mwanamuziki wa kufoka Kanye west kuandaa(produce) albam ya mwanachama wa
kundi la young money Tyga...

Lil Wayne
"Kwanini Tyga hakunipa taarifa kabla ya kukubaliana na Kanye!?" ni swali
analojiuliza Lil wayne akiwa kama mmiliki wa kundi alilopo Tyga... Tyga
mwenyewe anasema kuwa "kila nilipokuwa nakutana na Kanye West kwenye
starehe au popote ni kama tuna uunganiko fulani hiv.." na hapo ndipo hamu
ya Kanye west na Tyga kupata nafasi ya kujadili kufanya albam ya "GOLD".

Kanye West
 Lakini mwisho wa siku Lil wayne afunguka na kusema "hapana bwana kijana
anapambana kwaiyo tumuache afanye anachoona ni sawa" kwa kusema hivo
inaonyesha kuwa Rapper huyo kukubaliana jambo hilo kiroho safi japo
hakupewa taarifa kabla... kaa mkao wa kula kwani albamu ya GOLD njiani.

Tyga

CHRIS BROWN KUFUNGWA JELA

                                       CHRIS BROWN KUFUNGWA JELA
 Mwanamuziki kutoka nchini Marekani Chris Brown akamatwa na polisi
katika mji wa Malibu,california ambapo alikuwa matibabu au ushari wa
kuzuia au kujirekebisha na hasira ndani ya mienzi minne.. kwa sasa Chris
Brown anashikilia na polisi bila mzamana kwenye jela za Los Angeles,
Inmate Reception center...

Chris Brown akishikiliwa na polisi california
Kisa kikubwa cha mwanamusiki huyo kukamatwa na polisi hakijajulikana mpaka
sasa, kwa tetesi za watu wa karibu na msanii huyo kuwa kisa ni ugomvi na
madawa ya kulevya ndio sababu ya kukamatwa msanii Chris Brown.

Chris Brown
Mwezi jana katika moja ya kesi za msanii huyo ilisibitishwa kuwa Chris Brown
kuwa anamatatizo ya msongo wa mawazo na kushindwa kulala pia mahakama ili
msifu msanii huyo kwa kuwa mtii na kukubaliana na "community service"

BEYONCE ATOA VIDEO MPYA "PARTITION" BEHIND THE SCENES

           BEYONCE ATOA VIDEO MPYA "PARTITION" BEHIND THE SCENES
 Muongozaji wa video Jake Nava aingelea video hiyo na jinsi
anavyo fanya kazi na mwanadada Beyonce.Nava asema"inawezekana ikaonekana
kuwa video hii haina juhudi ndani...lakini Beyonce anatia bidii sana katika
kutengeneza video zake"...

Beyonce ndani ya video mpya ya "partition"

Malengo ya video hiyo ni uonesha jinsi mahusiano ya mwanadada Beyonce na mumewe
Jay z, kuwa ni mfano mzuri wa mahusiono ya kazi na mapenzi kufanikiwa kwa
kiasi kikubwa zaidi.Wimbo wa "partition" ndio wa mwisho kutengeneza katika albam
ya mwisho ya Beyonce... mpaka sasa albam hiyo kuuza zaidi ya nakala millioni mbili

Cover la album ya Beyone

Friday, March 14, 2014

KENDRICK LAMAR,PHARRELLI WILLIAMS AND ALICIA KEYS NDANI YA "AMAZING SPIDER MAN 2"

       KENDRICK LAMAR,PHARRELL WILLIAMS AND ALICIA KEYS NDANI YA
                                                  "AMAZING SPIDER MAN 2"
     "It's on again" jina la track hiyo iliyopewa na shujaa wa filamu
ya "amazing spiderman 2" Flick na vocal kuingizwa na Alicia Keys pamoja
na mwanamuziki aliye tikisa kwa wimbo wa "happy" Pharrell Williams,
Kendric lamar kumalizia na vina katika sound track hiyo...

Kendrick Lamar,Alicia Keys na Pharrell Williams

 Zimmer muaandaaji wa muziki mkongwe na Production ya Pharrelli Williams
kusimamia mzigo huo... "hii ndio collabor la nguvu, halijawahi tokea.."
maneno ya Alicia keys kwa kuwa nyimbo hio imebeba ujumbe na maudhui ya
Amazing spider man 2 na pia kwasababu kuna hali ya ushujaa ndani ya
wanamuziki hao watatu..

Muonekano wa Amazing spider man 2
 Pharrell Williams anasema wakati wa kutengeneza track hiyo alijua tuu
lazima Kendrick Lamar ahusike kwenye track hiyo kutokana na uzowefu wake
kwenye kutengeza soundtrack za filamu kwani moja ya soundtrack kwenye
katuni ya "Dispicable me" kugombea tunzo za oscar....
Producer wa filamu ya Amazing spiderman 2 anawaambia wapenzi wasubiri
kwa hamu kwani la leo ni zaidi ya jana.


Pharrell Williams

Thursday, March 13, 2014

ROBIN THICKLE NA PAULA PATTON NDOA YAKAA "MGUU PANDE"

ROBIN THICKLE NA PAULA PATTON NDOA YAKAA "MGUU PANDE"
     Miangaiko ya Robin Thickle kuweka ndoa sawasawa itafanikiwa!?
ni swali ambalo lipo kwa wapenzi "fans" wa mastaa hawa wa muziki na
filamu baada ya ndoa ya Robin na Paula kuteteleka mpaka kufikia..
kiasi cha kuchukua hatua ya kupeana taraka...
Wanandoa hao Robin Thickle na Paula Patton

      Habari kutoka kwa watu wakaribu na wanandoa hao wanasema kuwa
inawezekana pia star wa muziki Robin Thickle atafanikiwa kupata au
kuweka ndoa yake sawa kwani mpaka sasa Paula Patton hajahajiri mtu
wa kusimsamia taraka yake mahakamani...

Robin Thickle akiwa na mkewe Paula Patton parting
Wanandoa hao wameamua kufanya mazungumzo kwanza kabla ya kufikia
hatua ya taraka. Wapenzi wa mastar hao wanapenda kuona ndoa yao
ikiwa poa na kwa sasa wanawaombea kila heri wafikie muafaka na sio
kutengana.

NYIMBO KUMI BORA "TOP TEN" WIKI HII HIZI HAPAA!

NYIMBO KUMI BORA "TOP TEN" WIKI HII HIZI HAPAA!
              "It's hard to not be happy for pharrell" kwan ameendelea 
kushikilia namba moja kwenye chart ya wiki hii na kuwatupa mbali
      wanamuziki wenzake kwa wimbo wake wa sasa kwa jina ni HAPPY..
CHART YA TOP TEN DUNIANI KWA

Wednesday, March 12, 2014

MC LYTE "FIRST LADY" WA HIP HOP DUNIANI

            Katika kipindi cha sikukuu ya wanawake duniani Mc Lyte alifanya utafiti wa wanawake shujaa,shupavu na wasio na uoga... bila kuhofia uchache wao  wakabadilisha HIP HOP kwani "HIP HOP is tough game, only the best survive"
MC LYTE

            Wanamuzi wa HIP HOP wa kike kuanzia kwa wakina Queen Latifha mpaka Nikki Minaj wamevunja record na kuwa mashujaa "regends" wa HIP HOP kwa nguvu zoa wenyewe bila kujali jinsia wala iana ya muziki, Lakini hakuna hata mmoja anaye weza kujifananisha na MC Lyte njia alizo pita na mabadiliko aliyo yafanya na anayo yafanya mpaka sasa.
  1. Nikki Minaj akiwa na Queen Latifah katika pozi la pamoja

 
Blogger Templates